user_mobilelogo

Party Emblem

sdp party emblem

Party Headquarters

Swiss Cottages,House No.8 Ring Road,
Kileleshwa, Off Riverside Drive, Nairobi.
TEL: +254 721 276 829 / +254 745 124 425

Contact Us

Communist Party of Kenya (CPK)
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.

 

Find us on Facebook

sdpkenya facebook

Find us on Twitter

Important links

donate

 

membership

 

 

 

 

 

 

Tuwakumbuke

Mashujaa wa nchi yetu

Wazalendo halisi wa Kenya

Jinsi walivyokuwa wamejitolea mhanga

Kupambania uhuru na ukombozi wa nchi yetu:

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Tuwakumbuke mashujaa wa Pwani ya nchi yetu

Wazalendo wa Mombasa na Malindi na Lamu

Na Siu na Pate na Vanga....

Ambao mamia ya miaka iliyopita

Walikufa wakipambana

Wakipambana dhidi ya uvamizi wa Waarabu

Waliokataa kutawalwa na wageni

Walioupiga vita uvamizi wa kikatili wa Wareno

Wareno wakashindwa kabisa kupenya hadi bara

Tukumbuke kuwa ngome

Inayoitwa Fort Jesus

Ambayo sasa ni jumba la ukumbusho Mombasa

Ngome ni taswaira ya uvamizi wa Wareno nchini

Ni ushahidi wa upinzani kutoka kwa mababu na mabibi zetu

Ni ukumbusho wa nyanyaso na gandamizo

Za Wazungu wa kwanza kujaribu kutawala Kenya

Ngomeni maelfu ya Wamijikenda na Waswahili walifungwa

Ngomeni wazalendo wa nchi yetu waliteswa

Ngomeni damu ya mashujaa ilimwagika

Tumtaje Shee Mvita, mfalme wa mwisho wa Mombasa

Alieuawa na Wareno

Akiutetea uhuru na ukombozi wa watu wake

Mfano wa bei ghali iliyolipwa na wazalendo

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mwangeka

Wawa Mwangeka wa Mwanda Njawuli

Mzalendo kutoka Vuria,

Kilele cha milima ya Dawida

Milima ya juu zaidi Mashariki mwa Kenya

Inayosifika kwa uzuri wake usiyo na kifani

Ing'oni Mwangeka mzaliwa sehemu hii ya nchi yetu

Nae anatajika, ni mtu mashuhuri

Kwa uzalendo na ushujaa

Kwa kuongoza maaskari hodari wa Dawida

Waliowaeleza wakoloni kwa nyuta na mishale

Nyinyi ni nani mnaotamba katika nchi yetu?

Hii ni ardhi yetu kutoka kale na zamani

Tutaitetea hata kwa damu kumwagika

Tunapinga kutawalwa na wageni

Tuko kwa nchi yetu tunawezaje kuwafanyia kazi?

Tunaishi kwa jasho letu wenyewe

Basi itakuwaje tuwe wapagazi wezu?

Tu watu kama nyinyi tutakubalije kuwa watumwa wenu?

Tuna lugha, dini, mila na tamaduni zetu hatuna haja na zenu!

Kina Mwangeka wakatangaza vita dhidi ya vita vya wakoloni

Wakapigana wakapigana wakapigana bila kurudi nyuma

Mwangeka na maing'oni wa Dawida

Wakakataa kufa wakipiga magoti

Wakadinda kuwainulia maadui mikono yao

Wakafa wakiwa na silaha mikononi

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Halafu kuna Me Kitilili

Me Kitilili Me Kitilili Me Kitiliii

Me Kitilili wa Menza

Me Kitlili mwanamke shujaa kutoka Ugiriamani

Mzalendo Me Kitilili na Wanje, Wanje wa Mwadorikola

Jazanda ya uzalendo wa wanawake wa nchi yetu

Waliowaongoza wanaume na wanawake wa Ugiriamani

Kuuasi na kuulani ukoloni kwa maneno na vitendo

Kukataa kuwa maaskari wa wakoloni

Kugoma kufanywa mahamali wa mabeberu

Kudinda kunyang'anywa ardhi yao

Wakoloni wakawashambulia kikatili kikoloni

Wanje wa Mwadorikola na Mee Kitilili

Wakawaongoza wanaume kwa wanawake

Kutetea mila na tamaduni za Wagiriama

Kulinda hadhi ya mtu mweusi, heshima ya Mwafrika

Wakoloni wakawaita wanawake mashujaa wetu wachawi

Wakakashifiwa wakakamatwa wakadunishwa wakateswa

Mama zetu wakahamishwa hadi nchi ya Wakisii

Bali Me Kitilili na Wanje wa Mwadorikola

Wakasimama madhubuti wasitingishike wasikate tamaa

Wakatoroka na kujasiri mamia ya kilometa

Wasiogope hatari za nyika na misitu na wanyama tilatila

Wakarudi Ugiriamani kuendelea na mapambano

Wakaendelea kuongoza harakati dhidi ya ukoloni

Wakatukanwa wakapakwa matope wakazuiwa wakafungwa

Wakahamishwa hadi Kisimayu

Bali mama zetu milima ya ushujaa na uzalendo

Mfano wa ukakamavu na kujitolea mhanga

Wakakataa kusalimu amri za wakoloni

Wakatetea uhuru wa nchi yetu na watoto wao daima

Wakaishi wakiwa mihimili ya umoja wa watu wao

Wakawa sehemu ya nguzo ya historia ya ukombozi wa Kenya

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Huko Unandini Koitaleli ni mashuhuri

Koitaleli, kiboko cha kiburi cha wakoloni

Wanandi kwa mikuki na ngao mikononi

Wakawauliza wakoloni:

Hii ni nchi yetu kutoka tangu na tangu

Nani amewaruhusu kujenga reli hapa?

Mnawezaje kuingia na kupita kwetu

Bila hata hodi wala hamjambo!?

Mna njama gani juu ya ardhi yetu

Ambapo tumekuwa tukiishi tangu kale na zamani!?

Wakoloni kwa kiburi kujitapa na kujisahau

Wakajibu kwa bunduki na bomubomu

Kwa kuua na kuchinja pasina kutangaza vita

Wanandi wakatahamaki wakajizatiti sawasawa

Wakasema hawa watu ni wa sampuli gani?

Watu gani hawa wasio na heshima wala adabu!

Ni binadamu gani hawa wasiojali maisha?

Hawajui lugha nyingine ila vita na madharau tu!

Basi, imetupasa kupigana nao

Kwani nasi hatuna utamaduni wa woga

Ndipo Wanandi wakajiandaa ipasavyo

Kwa mikuki na ngao wakajumuika

Mabingwa wa vita vya kigorila wakajipanga barabara

Wakawa wanawavizia na kuwashambulia ghaflaghafla wachokozi

Kina Koitaleli wakawachapa wavamizi hadi wakasarenda

Wakatapika kiburi chao wakaomba majadiliano

Mwafrika, mtu mweusi, akawafanya wainue mikono

Ikawa hawana budi ila kuitisha majadiliano ya amani

Ela Koitaleli alipoenda kujadiliana na mabeberu akauawa

Shujaa Koitaleli akauawa kwa mizungu ya Wazungu ya kioga

Bali kina Semoi wakachukua nafasi yake

Mapambano dhidi ya ukoloni yakaendelea

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Tunajivunia Waiyaki

Waiyaki Waiyaki Waiyaki

Waiyaki wa Dagoreti

Chimbuko cha mapambano ya Wakikuyu dhidi ya walowezi

Damu iliyozaa Jeshi la Uhuru na Mashamba, Mau Mau

Kina Waiyaki walipinga unyonyaji wa makampuni ya kibeberu

Walisema hapana kwa ubepari nchini

Hapana kwa mfumo wa kiuchumi wa unyonyaji wa mtu kwa mtu

Walivamia ngome za kupanda mizizi ya mirija ya ubeberu Kenya

Wazalendo wa nchi yetu waliasi kupunjwa na wageni

Wakakataa na utu wa Mwafrika kwa silaha

Waiyaki akakamatwa kuhamishwa Pwani

Wakamshawishi wakamtisha wakamtesa ili asarende

Wapi! wakapiga ukuta kwa babu yetu

Wakashindwa kuumwaga uzalendo wa Mkenya halisi

Wasiweze hata kuukwaruza uhodari wake

Ufashisti wa wakoloni ukazidi kudhihirika Kibwezi

Walipomzika shujaa wetu Waiyaki akiwa hai

Miungu ya nchi yetu

Waingereza walimzika mzalendo akiwa bado anaishi!

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Nyanjiru

Oh Nyanjiru

Tumkumbuke Mary Muthoni Nyanjiru

Yule mwanamke jasiri wa enzi za kiburi cha walowezi

Nyakati za ushujaa wa Harry Thuku

Siku za kukataa kubeba vipande vya wakoloni

Kudinda kulazimishwa kuwafanyia kazi masetla

Kugomea mishahara duni ya kitumwa

Kupinga kunyonywa na kunyanyaswa kwa wanawake

Enzi za chimbuko cha vyama vya kupigania uhuru

Hizo enzi za East African Association

Mapambano ya wafanyikazi katika miji ya nchi yetu

Mapambano dhidi ya kina Colonel Grogan na Lord Delamare

Wakati unyama wa wakoloni dhidi ya wananchi

Ulikuwa ni sehemu ya maisha ya kila siku

Tukitukanwa na kufungwa na kuteswa kiholela

Tukitemewa mate na Wazungu vururumtende

Tukidhihakiwa na kudhalilishwa

Na kina memsahibu walokuwakitamba mijini na mashambani

Sisi watu weusi tukifanywa watu wa mwisho

Kana kwamba Kenya si nchi yetu wenyewe

Hizo nyakati za kupinga kulipa kodi kwa wavamizi

Harry Thuku akakamatwa na kuwekwa ndani

Wanaume na wanawake wa Nairobi wakaandamana

Harry Thuku na wafungwa wote wa kisiasa wawachiliwe!

Wafunguliwe mara moja tena bila masharti!

Nje ya Norfolk Hotel

Karibu na Chuo Kikuu cha Nairobi

Si mbali na Central Police Station

Siku hiyo mwaka wa 1922

Kina Nyanjiru walikata shauri kuandamana hapo

Hadi shujaa wao atakapofunguliwa

Wakalala hapo kwa siku na masiku

Baridi ya usiku wakivumilia na njaa na kiu pia

Vitisho vya walowezi wasikubali viwatishe

Bezo za kishenzi za kuuzi za wavamizi wakazipuuza

Na hata wanaume walipozubaa na kusitasita

Walipolegalega na kushindwa kutoa uongozi thabiti

Mary Muthoni Nyanjiru hakulimatia, alijitokeza kimoja

Akadai wanaume wavue surwale na kuvaa skati

Wawape wanawake surwale zao wazivae

Ndipo wanawake wakawa katika msitari wa mbele

Wanaume wakifuata nyuma katika harakati za ukombozi

Pamoja wakasonga mbele kumfungulia mpendwa wao

Pamoja wakaandika historia ya uhuru wetu-kwa damu yao

Shujaa Mary Muthoni Nyanjiru

Akawa wa kwanza kuangushwa na risasi za polisi wa kikoloni

Makaburu waliokuwa wakistarehe Norfolk Hotel

Huku wakiwatukana na kuwakebehi watu wetu

Wakachukua silaha zao kwa furaha za wehu

Wakaungana na polisi wao kufanya mito ya damu Nairobi

Kutoka kwa mamia ya dada na kaka zetu

Bali yote hayo hayakuzima moto wa mapambano ya uhuru

Ukaendelea kuwaka moto wa uhuru ukazidi kuzagaa

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Tumkumbuke Makhan Singh

Komredi Makhan Singh, mkomunisti wa kwanza Kenya

Sehemu ya harakati za wafanyikazi dhidi ya ukoloni

Sogora wa mbinu na hila za kuzatiti mapambano

Mapambano ya wavujajasho dhidi ya mabepari

Katika historia ya vyama vya kimaendeleo vya wafanyikazi

Jina la mwanamapinduzi Makhan Singh litang'aa daima

Makhan Singh, sehemu ya kina Chege Kibacia

Chege Kibacia na mashujaa wa watiririkajasho

Makhan Singh,alieaminika hata KAU ya Kiburi House

KAU ya Mau Mau katika Kiburi House

Ndiyo, tusisahau Kiburi House

Kiburi House, walikokuwa wakikutana kina Bildad Kaggia

Kina Eliud Mutonyi na kina Isaac Gathanju

Kiburi House, kulikokuwa kukipangwa njama za Mau Mau

Ngome ya waliochagua barabara ya mapinduzi

Walimtambua Makhan Singh Kiburi House walimhesabu

Kina Makhan Singh na Pio Gama Pinto na Alibhai Mulla Jeevanjee

Wazalendo wa Kenya wa asili ya Kihindi

Waliowaambia Wahindi wa Kenya

Enyi wananchi wenzetu wa asili ya India

Tahadharini msiwe mapopo na vinyonga

Epukaneni na kuwa makupe na makunguni wa nchi hii

Ikiwa Kenya ni nchi yenu

Kama mnajihesabu raia wa nchi hii

Unganeni na Wafrika kupigania uhuru wa Kenya

Kuweni sehemu ya wazalendo wanaodai ukombozi

Msikubali kutumiwa kunyonya na kufukarisha taifa hili

Kataaeni kuwa upande wa wakoloni na wadhalimu

Msijidanganye kuwa nyinyi ni bora kuliko wenyeji

Wafanyikazi wote tunanyonywa haya shime tuungane

Tuwe na mshikamano dhidi ya wanyonyaji

Tusikubali ubaguzi wa rangi utuvunjie umoja wetu

Tuugomee ukabila usitumiwe kuondoa uwezo wetu

Wala tusikubali migawanyiko ya kijinsia iturudishe nyuma

Kenya na Uganda na Tanzania wafanyikazi tuwe kitu kimoja

Wafanyikazi wote tupambanie taifa la Afrika Mashariki

Afrika Mashariki ya kimapinduzi

Afrika Mashariki inayopinga ukoloni-mamboleo

Afrika Mashariki ya mfumo kwa kisoshalist

Afrika Mashariki itakuwa nguvu kubwa za kisiasa na kiuchumi

Afrika Mashariki itakuwa matumaini ya uhuru na ukombozi kamili

Sauti ya Makhan Singh, sauti ya wanaonyanyaswa

Iliyoitikiwa na wafanyikazi na umma wa wazalendo

Iliwafanya wakoloni kujikojolea na kujiharia

Makhan aliwakosesha mabepari wa Afrika Mashariki usingizi

Jina lake likaandikwa katika kitabu cheusi cha dola la kikoloni

Na hali ya hatari ilipotangazwa rasmi

Makhan Singh hakusahauliwa na kifagio cha polisi wa kikoloni

Makhan Singh alikamatwa mara moja

Makhan Singh akafungiwa kizuizini

Makhan Singh alifungwa miaka kumi kizuizini

Kwa sababu ya harakati za wavujajasho alifungwa Makhan Singh

Alifungwa kwa ajili ya uhuru wa taifa letu

Bali bendera ya wakoloni iliposhushwa Kenya

Na bendera ya Wakenya kupandishwa

Kupandishwa na mapambano ya kina Makhan Singh

Serikali ya msaliti Jomo Kenyatta na mahomugadi

Ilimchukuwa Makhan kana kwamba si lolote si chochote nchini

Bali kutambuliwa na wanyapara wa mitaji ya mabeberu Kenya

Kupigana pambaja na wanyonyaji na wagandamizaji wa wafanyikazi

Haikuwa nia ya komredi Makhan Singh, mwanamapinduzi

Makhan Singh alikufa akiandika historia ya mapambano

Historia ya mapambano ya wafanyikazi wa Kenya

Makhan Singh ....Makhan Singh....Makhan Singh.......

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu tilatila

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mau Mau

Mau Mau, jeshi la Uhuru na Mashamba

Kilele cha mapambano dhidi ya ukoloni-mkongwe

Jazanda ya wazalendo na uzalendo

Mau Mau, mashujaa halisi wa nchi yetu

Wakakataa kutembea katika njia ya kina Jomo Kenyatta

Njia ya wasabili ya kuomba uhuru wa kuomba

Njia ya kutegemea adili ya wagandamizaji

Njia ya kuongozwa na masilahi ya ulafi na uroho

Njia ya kukana mapambano ya silaha katika hali ya ufashisti

Mau Mau wakulima na wafanyikazi wa Kenya

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Walichagua barabara ya kimapinduzi ya uhuru

Mau Mau waliokula kiapo cha ukombozi

Kiapo cha kuwaunganisha na kuwashikanisha kwa mapambano

Mapambano ya kupigania mashamba na uhuru wetu

Mapambano ya kupigania heshima na utu wa mtu mweusi

Mapambano ya demokrasi na haki za binadamu

Mapambano ya kuung'oa ukoloni nchini kwetu

Maelfu kwa maelfu ya wazalendo wa Kenya

Waliowacha kila kitu na kuitikia mwito

Mwito wa kujitoma milima Kenya na Nyandarua

Mwito wa kusambaa katika miji na vijiji vya nchi yetu

Kuendeleza vita vya kigorila dhidi ya wakoloni na vibaraka vyao

Waliovumilia njaa na kiu na baridi na upweke na dhiki tilatila

Wakajasiri kuwindwa na kukamatwa na kuhamishwa

Waliokuwa tayari kuvumilia kukamatwa na kufungwa

Mau Mau, maelfu kwa maelfu waliwawa na wakoloni

Mau Mau, ni wangapi mashujaa wetu waliyonyongwa!

Mau Mau, kiboko cha makaburu na mahomugadi

Mau Mau, kwa damu yenu, kwa kujitolea mhanga kwenu

Enyi wananchi wakereketwa wa taifa letu

Kwa msimamo wenu

Kwa mwelekeo wenu

Kwa harakati zenu

Kwa vita sahihi mlivyopigana

Tuko pahali tulipo sasa, hatua kubwa mbele

Ukoloni-mkongwe haupo tena nasi, mliukwamua Mau Mau

Kwenu Afrika ikapata mfano mzuri wa kuiga

Mfano wa kupigania ukombozi kwa kutumia silaha

Mau Mau, Jeshi la uhuru na Mashamba

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mau Mau

Vilikuwa vita vya kupigania uhuru wa kitaifa

Vita vya wananchi na wananchi kwa ajili ya wananchi

Navyo vita vya wananchi vilizaa mashujaa wengi, wengi sana

Mashujaa waliochipuka katika msitari wa mbele

Mashujaa walioteuliwa na ari na shauku ya kujitolea mhanga

Kujitolea mhanga kutumikia vita vya ukombozi

Mashujaa waliodhihirisha ujemedari na uhodari

Wa kuongoza jeshi lililokuwa la wananchi wa Kenya

Mashujaa waliokuwa mashuhuri katika uwanja wa vita

Kwa usanii wa kuzalisha hila na mbinu za kuwachapa maadui

Mashujaa wa siasa na itikadi ya wanaonyanyaswa

Waliohamasisha umma kwa maneneo na vitendo vyao

Mashujaa wa kutetea haki na ukweli na maslahi ya wengi

Waliochagua kuishi maisha ya utu ya kupinga dhuluma

Mashujaa kwa mapenzi ya nchi yetu na ukombozi wake

Kwa maendeleo ya Kenya na furaha  ya kila raia

Kwa imani na amani ya wanaonyonywa na kunyanyaswa

Mashujaa waliokuwa wakipiga konde nyoyo kila wakati

Waliopambana dhidi ya kulegalega na kukata tamaa

Mashujaa ambao baada ya kukamatwa na wakoloni

Wakiwa mikononi mwa makaburu na mahomugadi

Wakiteswa katika magereza ya wadhalimu wa nchi yetu

Katikati ya ufashisti wa dola la Waingereza

Walivumilia yote kwa ujasiri usiyo na kifani

Walikataa kusaliti kiapo cha kupigania uhuru

Wakadinda kukana vita vya haki vya ukombozi wa Kenya

Wasikubali kutoboa siri wala kusaliti makomredi wao

Na hata waliponyongwa na kuuawa kinyama kabisa

Mashujaa wetu walikufa kwa fahari

Wakawawachia wakoloni na vibaraka wao aibu ya milele

Ni wengi mashujaa wa Mau Mau, wengi sana

Kwani Mau Mau ni wanati, wananchi wazalendo wakereketwa

Mau Mau, ushujaa wa mamilioni

Ya wakulima na wafanyikazi

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Ambao kwa moyo wa harambee uzalendo na kujitegemea

Walifunga sura  ya ukoloni-mkongwe katika nchi yetu

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

Challenging Imperialism: Communist Party of Kenya and the Left Alliance for Nati...
16 Apr 2024 17:21

The Communist Party of Kenya and the Left Alliance for National Democracy and Socialism (LANDS) demand that the Kenya Kwanza government and Jamaica Labour Party rescind their commitment to lead and participate in a deployment of armed personnel to Haiti. We call on the Kenyan and Jamaican people to join the Haitian masses and popular progressive forces worldwide in opposing the intervention, continued occupation and neo-colonial governance of Haiti by the Core Group[1] and the UN. We oppose the actions of CARICOM members, following a meeting in Jamaica that included the USA, France and Cana [ ... ]

Read more
Doctors' Strike: President Ruto's Hypocrisy Exposed
12 Apr 2024 11:59

The Communist Party of Kenya stands in resolute solidarity with the striking doctors and workers across Kenya, condemning the bourgeoisie state's flagrant disregard for the rights and well-being of the working class.  President Ruto's administration, serving the interests of big capital, has prioritized the enrichment of the elite while neglecting the basic needs of the people. President Ruto's plea for doctors to "live within our means" while simultaneously pandering to big capital is a stark display of hypocrisy. While urging austerity measures on the working class, his administration has  [ ... ]

Read more
Honouring the Lao People’s Revolutionary Party: A Testament to Socialist Resilie...
03 Apr 2024 10:34

In the annals of revolutionary history, the Lao People’s Revolutionary Party (LPRP) stands as a beacon of unwavering commitment to socialist principles and the liberation of the working class. From its humble beginnings to its present-day leadership, the LPRP has demonstrated resilience, unity, and an unyielding dedication to the betterment of the Laotian people. As comrades of the Communist Party of Kenya (CPK), we proudly extend our heartfelt homage to our counterparts in Laos on the occasion of the anniversary of their party’s founding. The inception of the LPRP on 22nd March 1955 mark [ ... ]

Read more
Solidarity Statement with the Party of Communists USA
03 Apr 2024 10:33

  Dear Comrades, With revolutionary fervor and unwavering commitment to the global proletarian struggle, we, the Central Organizing Committee of the Communist Party of Kenya, extend our heartfelt solidarity to the Party of Communists USA as they convene for their 3rd Congress, commemorating the 10th anniversary of their party's founding. Though geographical distances may separate us, our revolutionary spirits are united in the noble cause of emancipating the working class from the shackles of imperialism and capitalist exploitation. The Party of Communists USA has long been a stalwart defe [ ... ]

Read more