user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Mau Mau

Mau Mau, jeshi la Uhuru na Mashamba

Kilele cha mapambano dhidi ya ukoloni-mkongwe

Jazanda ya wazalendo na uzalendo

Mau Mau, mashujaa halisi wa nchi yetu

Wakakataa kutembea katika njia ya kina Jomo Kenyatta

Njia ya wasabili ya kuomba uhuru wa kuomba

Njia ya kutegemea adili ya wagandamizaji

Njia ya kuongozwa na masilahi ya ulafi na uroho

Njia ya kukana mapambano ya silaha katika hali ya ufashisti

Mau Mau wakulima na wafanyikazi wa Kenya

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Walichagua barabara ya kimapinduzi ya uhuru

Mau Mau waliokula kiapo cha ukombozi

Kiapo cha kuwaunganisha na kuwashikanisha kwa mapambano

Mapambano ya kupigania mashamba na uhuru wetu

Mapambano ya kupigania heshima na utu wa mtu mweusi

Mapambano ya demokrasi na haki za binadamu

Mapambano ya kuung'oa ukoloni nchini kwetu

Maelfu kwa maelfu ya wazalendo wa Kenya

Waliowacha kila kitu na kuitikia mwito

Mwito wa kujitoma milima Kenya na Nyandarua

Mwito wa kusambaa katika miji na vijiji vya nchi yetu

Kuendeleza vita vya kigorila dhidi ya wakoloni na vibaraka vyao

Waliovumilia njaa na kiu na baridi na upweke na dhiki tilatila

Wakajasiri kuwindwa na kukamatwa na kuhamishwa

Waliokuwa tayari kuvumilia kukamatwa na kufungwa

Mau Mau, maelfu kwa maelfu waliwawa na wakoloni

Mau Mau, ni wangapi mashujaa wetu waliyonyongwa!

Mau Mau, kiboko cha makaburu na mahomugadi

Mau Mau, kwa damu yenu, kwa kujitolea mhanga kwenu

Enyi wananchi wakereketwa wa taifa letu

Kwa msimamo wenu

Kwa mwelekeo wenu

Kwa harakati zenu

Kwa vita sahihi mlivyopigana

Tuko pahali tulipo sasa, hatua kubwa mbele

Ukoloni-mkongwe haupo tena nasi, mliukwamua Mau Mau

Kwenu Afrika ikapata mfano mzuri wa kuiga

Mfano wa kupigania ukombozi kwa kutumia silaha

Mau Mau, Jeshi la uhuru na Mashamba

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mau Mau

Vilikuwa vita vya kupigania uhuru wa kitaifa

Vita vya wananchi na wananchi kwa ajili ya wananchi

Navyo vita vya wananchi vilizaa mashujaa wengi, wengi sana

Mashujaa waliochipuka katika msitari wa mbele

Mashujaa walioteuliwa na ari na shauku ya kujitolea mhanga

Kujitolea mhanga kutumikia vita vya ukombozi

Mashujaa waliodhihirisha ujemedari na uhodari

Wa kuongoza jeshi lililokuwa la wananchi wa Kenya

Mashujaa waliokuwa mashuhuri katika uwanja wa vita

Kwa usanii wa kuzalisha hila na mbinu za kuwachapa maadui

Mashujaa wa siasa na itikadi ya wanaonyanyaswa

Waliohamasisha umma kwa maneneo na vitendo vyao

Mashujaa wa kutetea haki na ukweli na maslahi ya wengi

Waliochagua kuishi maisha ya utu ya kupinga dhuluma

Mashujaa kwa mapenzi ya nchi yetu na ukombozi wake

Kwa maendeleo ya Kenya na furaha  ya kila raia

Kwa imani na amani ya wanaonyonywa na kunyanyaswa

Mashujaa waliokuwa wakipiga konde nyoyo kila wakati

Waliopambana dhidi ya kulegalega na kukata tamaa

Mashujaa ambao baada ya kukamatwa na wakoloni

Wakiwa mikononi mwa makaburu na mahomugadi

Wakiteswa katika magereza ya wadhalimu wa nchi yetu

Katikati ya ufashisti wa dola la Waingereza

Walivumilia yote kwa ujasiri usiyo na kifani

Walikataa kusaliti kiapo cha kupigania uhuru

Wakadinda kukana vita vya haki vya ukombozi wa Kenya

Wasikubali kutoboa siri wala kusaliti makomredi wao

Na hata waliponyongwa na kuuawa kinyama kabisa

Mashujaa wetu walikufa kwa fahari

Wakawawachia wakoloni na vibaraka wao aibu ya milele

Ni wengi mashujaa wa Mau Mau, wengi sana

Kwani Mau Mau ni wanati, wananchi wazalendo wakereketwa

Mau Mau, ushujaa wa mamilioni

Ya wakulima na wafanyikazi

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Ambao kwa moyo wa harambee uzalendo na kujitegemea

Walifunga sura  ya ukoloni-mkongwe katika nchi yetu

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Kimaathi

Dedan Kimaathi

Dedan Kimaathi wa Waciuri

Mkuu wa jeshi la Uhuru na Mashamba

Kati ya majemedari wa Mau Mau Kimaathi ali ni gogo

Baina ya mashujaa wa uhuru hakika Dedan Kimaathi ni nyota

Nyota iliyoonekana na inayoonekana katika kila pembe ya Kenya

Nyota inayong'aang'aa Afrika kuonyesha barabara sahihi

Barabara ya kimapinduzi ya kuelekea kwa uhuru

Nyota mashuhuri Afrika na hata duniani kote

Kwa wanaonyonywa na kugandamizwa

Oh pande la mwana wa Kenya, ndugu yetu mpendwa Kimaathi

Ni maneno gani tutayatumia  ewe mwana wa Waciuri

Hata tukaeleza  sifa zako tilatila kwa kikamilifu?

Ninashindwa hata kupata nahau bora

Za kuandika kuhusu Mkuu wa Jeshi la Uhuru na Mashamba

Pengine niseme tu kuwa Kimaathi alikuwa mtu

Alikuwa mtu Kimaathi, mtu kama sisi

Alikuwa na mamaye na babaye na bibiye na babuye

Alikuwa na jamaaze, damuye, kama sisi

Alikuwa na mke, mke aliempenda sana, tena sana

Kimaathi alikuwa kijana, kijana  kama sisi

Kijana alietambua jukumu lake kama mwananchi mzalendo

Mtu ambae alifahamu yu mtu kwa maneno na matendo

Kimaathi, maana ya mapenzi kwa nchi yako na watu wake

Kimaathi, mfano halisi wa ushujaa wa kimapinduzi

Ushujaa wa umma uhodari wa maslahi ya wanaogandamizwa

Kimaathi, twasira na jazanda ya kujitolea mhanga

Kwa uhuru na ukombozi wa kitaifa

Kati ya wasanii wa hila na mbinu ya vita vya kigorila

Kimaathi wa Waciuri anatajika kama msanii mkubwa

Kati ya majina yaliyokuwa yakiogopewa na wakoloni

Jina la Dedan Kimaathi lilikuwa namba wani

Kimaathi aliwafanya makaburu kujikojolea na kujiharia

Wanyonyaji wakashindwa kula manyonyaji yao kwa amani

Wangapi walowezi walifungasha na kuondoka

Kwa kuogopa Kimaathi, asakari hodari wa Mau Mau!

.....ahhhh! lakini nani asiemfahamu Kimaathi nchini!

Ni mwananchi gani mzalendo ambae hajui Mau Mau!

Ni historia gani ya Kenya hiyo ambayo haitaji Mau Mau!

Ni mashujaa gani wa Kenya unawajua kama humjui Kimaathi!

Hakika katika kuandika historia sahihi ya taifa letu

Hatutawasamehe kina Ndirangu Mau milele

Kina Ndirangu Mau- mahomugadi waliyomsaliti shujaa wetu

Kina Ndirangu Mau- kina Kenyatta na Moi wenye dola la kisaliti

Kina Ndirangu Mau- wanyonyaji wa wakulima na wafanyikazi

Kina Ndirangu Mau- vibaraka wa mabeberu

Kina Ndirangu Mau- wanaopinga ukombozi wa taifa letu

Tutawasemehe vipi kwa kuendelea kukataa kumzika Kimaathi!?

Mnamo tarehe 18  Februari, 1957

Katika Jela ya Nairobi

Dedan Kimathi wa Waciuri, shujaa mkuu wa Kenya

Alinyongwa na wakoloni wa Waingereza

Alinyongwa baada ya mateso ya kifashisti ya kina Ian Henderson

Alinyongwa huku akipambana akiwa na pingu mikononi

Shujaa wa nchi yetu alikufa akipigana

Mwili wa Kimaathi ulitupwa na wakoloni

Katika Jela ya Kamiti

Na hadi wa leo

Mazishi ya Mzalendo Kimathi

Yanangojea kufanywa, tukumbuke

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

Mwamdawiro Mghanga, Mwenyekiti wa CPK

                                                            Jela Kuu ya Kibos    04-06-198

 

  The Rural Woman: Not to Be Celebrated—But Liberated
24 Nov 2025 06:00

                                                                  peech on the Peasant Women Day, 15th October, 2025. Written by Leon Munala Secretary of The Peasants and Peasant Organization Delivered by Comrade Karimi Wa Kagendo National Organising Secretary, Revolutionary Youth League Comrades, sisters, and fellow workers! Today, the representatives of global capital in their glass palace tells us to celebrate. The United Nations, that grand committee for managing the common affairs of the global bourgeoisie, has  [ ... ]

Read more
FROM THE COMMUNE TO THE PEOPLE’S POWER: ANTI-IMPERIALIST STRUGGLE AND THE PATH O...
12 Nov 2025 08:41

    Booker Omole General Secretary, Communist Party Marxist Kenya (CPMK) October 17th, 2025 Caracas, Venezuela   omuna o Nada: The Question of Power in the Age of Imperialist War Comrades, the slogan “Comuna o Nada” — the commune or nothing — is not merely a Venezuelan proclamation; it is a universal cry of the proletariat in our epoch of crisis. It affirms that without transforming the relations of production, without uprooting imperialist domination, and without transferring power from the exploiting classes to the working people, there can be no socialism.   Today, [ ... ]

Read more
OFFICIAL STATEMENT ON THE FASCIST OFFENSIVE OF IMPERIALISM IN TANZANIA UNDER PR...
05 Nov 2025 14:01

November 2, 2025   The Communist Party Marxist Kenya stands with the people of Tanzania in this moment of heightened danger. The ruling class across East Africa is tightening the chains of monopoly finance capital. The mask of liberal democracy is falling. Behind it stands naked reaction. Behind it stands fascism in African colours.   President Samia Suluhu Hassan has presided over political developments marked by aggressive interference from foreign capital. We are witnessing new assaults by the corporations and financial institutions headquartered in the old imperial centres. They want [ ... ]

Read more
STATEMENT ON THE PASSING OF COMRADE KIM YONG NAM COMMUNIST PARTY MARXIST KENY...
05 Nov 2025 13:51

    November 5, 2025   The Communist Party Marxist Kenya conveys its deepest condolences to the Workers Party of Korea, the Government of the Democratic People’s Republic of Korea, and the heroic Korean people on the passing of Comrade Kim Yong Nam, former Chairman of the Standing Committee of the Supreme People’s Assembly.   Comrade Kim Yong Nam was not merely a statesman. He was a defender of sovereignty. He was a guardian of independence. He was a steadfast revolutionary in the global front against imperialism.   Throughout his service to the Party and the State, the Dem [ ... ]

Read more