user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

“Utekelezaji wa sera za kibepari nchini umetuumiza sisi wananchi tuliyo wengi. Ubinafsishaji wa ardhi, migodi, mbuga za wanyamapori na maliasili zingine umetupora sisi tuliyo wengi haki za umilikaji na matumizi ya ardhi zetu za jadi tulizozirithi kutoka kwa mabibi na mababu zetu. Badala yake serikali inashirikiana na wawekezaji (mabepari) wa nchini na wa kigeni kutunyonya, kutunyanyasa, kutuvunjia heshima, kuvuraga utamaduni wetu na haki zetu za binadamu kiholela. Mfumo wa ubepari na ubinafsishaji unaoendelea hauwezi kutukomboa kutoka kwa ufukara na kutuletea maendeleo endelevu kwani unapanua pengo kati ya matajiri na masikini. Lazima tujizatiti na kuungana kupambania kurudi kwa Azimio la Arusha!”.

Hayo na mengine yalisemwa na kuazimiwa na jamii za wakulima, wachungaji, mashirika ya umma na Watanzania makabwela ambao walishiriki katika Kongamano la Saba la tamasha ya wasomi ya kumuenzi baba wa taifa la Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kongamano hilo lililofanyika kutoka tarehe 13 hadi 15 Aprili mwaka huu katika Ukumbi wa Nkuruma katika Chuo Kikuu cha Dar - es - saalamu liliandaliwa na Kigoda cha Nyerere chuoni hicho chini ya uwenyekiti wa Profesa Peminah Mlama. Pamoja na watu kutoka mashinani, Kongamano hilo lilishirikisha wasomi na wanafunzi wa chuo kikuu na wa shule za upili ambao walilalamika jinsi wawoto wa makabwela wanavyozidi kunyimwa fursa ya kupata elimu bora kutokana na ubinafsishwaji wa taasisi za elimu nchini Tanzania. Wanafunzi wa chuo kikuu walilalamika kuhusu ukame wa demokrasi ya kitaaluma katika vyuo vikuu iliyoandamana na ubinafsishwaji wa elimu katika nchi hiyo. Kongamano hilo lilisisimuliwa na wanafunzi wa shule za upili waliyolalamika kwa ufasaha kuwa elimu sasa inawafundisha watoto maadili ya ubinafsi, ulafi na kutojali binadamu wengine badala ya yale ya kiutu na kizalendo yaliyokuwa yakifundishwa na mwasisi wa taifa lao, Nyerere.

Wawakilishi wa jumuia za wakulima na wachungaji kutoka Loliondo, Kilosa, Mbeya, Geita walieleza kwa uchungu kuhusu masaibu wanayolazimika kuishi nayo kutokana na kunyanyaswa na kuporwa haki juu ya ardhi na maliasili zao na wawekezaji wa Kitanzania na kigeni ambao sasa wanapendelewa na serikali dhidi ya jumuia. Kongamano lilisikitishwa na maelezo kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu za wakulima na wachungaji wanaoishi katika maeneo ya migodi ya Geita, Shinyanga na Mwanza. Kilio hichihicho kililiwa na wakulima makabwela wa mpunga kutoka Mbeya waliyonyang’anywa ardhi zao na wajasiriamali na serikali. Pia jumuia za wakulima na wachungaji za Kilosa katika Mkoa wa Morogoro zilisimulia jinsi dhuluma na migogoro ilivyozidi sehemu zao kutokana na uvamizi na unyakuzi wa ardhi unaoendelea kutokana na ubinafsishaji.

Aidha, wanaharakati wa kupigania haki za kijamii kutoka Kampala na Moroto Uganda walishiriki na vilevile mashirika ya umma ya Kenya mkiwemo shirika la haki za kijinsia, shirika la kupigania haki ya maji na shirika la kupigania haki ya ardhi ya umma huko Garissa. Nikiwa mwenyekiti wa chama cha Social Democratic Party of Kenya (SDP) niliongoza ujumbe wa wanachama wanne kushiriki kongamano hilo maarufu.

Mada kuu ya kongamano hilo ilikuwa ubinafsishaji na haki za kijamii. Shabaha ya mada hii ilikuwa ni kutathmini athari za kiuchumi, kisiasa, kijamii na kitamaduni za marekebisho ya kiuchumi yaliyotoa Tanzania kutoka barabara ya Azimio la Arusha (ujamaa) na kuitia katika barabara ya ubeparimamboleo. Baada ya Nyerere kung’atuka kutoka kwa urais wa Jamhuri ya Tanzania na pia uwenyekiti wa chama tawala, Chama cha Mapinduzi (CCM), rais Ali Hassan Mwinyi aliyechukua nafasi yake alianza marekebisho ya kiuchumi ya kibepari katika nchi hiyo. Rais Benjamini Mkapa alimrithi Mwinyi na kuendelea kuzingatia sera za Rais Mwinyi za ruksa ya kuuvunja mfumo wa ujamaa na kujitegemea na kuelekeza Tanzania katika mfumo wa ubepari. Hivi leo Tanzania ikiongozwa na Rais wa nne Jakayo Mrisho Kiketwe inaendelea kutekeleza sera za ubepari na ukolonimamboleo kwa fujo.

Huku ikiwa katika mfumo wa ubepari, uchumi wa Tanzania umekua kwa kasi sana (kwa zaidi ya asilimia saba). Barabara nyingi za lami zimejengwa mijini na mikoani. Katika kila miji ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Dar - es - saalamu, Dodoma, Tanga, Mbeya, Arusha, Mwanza na Moshi majumba makubwa ya ghorofa yanaota kila kuchako. Aidha, mitaa ya kifahari wanakokaa matajiri yenye majumba makubwa na ya kupendeza ajabu nayo pia ni dhihirisho la kunoga kwa uchumi wa ubepari. Vilevile, masupamaketi ya kukidhia haja za tabaka la mabwanyenye na magari ya kifahari yamejaa kila sehemu mijini. Ardhi, migodi na mashirika ya umma yamezidi kubinafsishwa na kuuziwa (kupewa) mabepari wa Tanzania na nchi za kigeni. Wawekezaji kutoka kila pahali ulimwenguni wanakimbilia Tanzania kuwekeza na kununua mali ya umma ya viwanda, biashara, ardhi, madini, wanyamapori na maliasili zingine. Hata huduma za elimu, nyumba, maji, afya na umeme zimebinafsishwa.

Je, utekelezaji wa sera za ubepari umeathiri vipi tabaka la makabwela wa Tanzania? Washiriki wa kongamano la Nyerere walisema na kukubaliana kuwa ubinafsishaji wa uchumi kwa ujumla ni kinyume cha haki kwani unachukua mali inayomilikiwa na serikali kwa ajili ya wengi (umma) na kuwapa watu binafsi kwa kisingizio kimoja ama kingine. Marekebisho ya ubepari yamezidisha pengo kati ya matajiri na maskini, kupanda mbegu za uhasama wa kikabila  na kukiuka maadili ya kiutu yaliyozingatiwa na azimio la Arusha. Rushwa imekuwa dondandugu huku unyonyaji wa mtu kwa mtu ukiwa utamaduni wa kisasa. Wakati tabaka la wachache wanaotawala wakijilimbikizia utajiri mkubwa ajabu tabaka la Watanzania wengi linazidi kudidimia katika lindi la ufukara, shida na umkosefu wa kila hali. Washiriki kutoka Kenya, Malawi, Afrika Kusini na Uganda pia walisisitiza kwamba ubinafsishaji wa uchumi katika nchi zao pia umeleta manufaa kwa tabaka la wachache tu huku tabaka la wengi likizidi kusukumwa pembeni. Mwishowe kongamano liliamua kuwa ubepari umefeli Tanzania na pia Afrika Mashariki. Watanzania wengi hawana budi kupigania kurudi kwa Azimio la Arusha la siasa ya ujamaa na kujitegemea.

 

Mwandawiro Mghanga, Mwenyekiti wa Social Democratic Party of Kenya (SDP), Aprili 22, 2015

THE DRIVE INTO WORLD WAR 3 AND THE WORLD ANTI IMPERIALIST FRONT
11 May 2026 07:14

  ate:  10b>th May 2026 Occasion: International Colloquium by World Anti-Imperialist Platform, Nairobi    Author: Booker Omole Position: General Secretary, Communist Party Marxist Kenya   E DRIVE INTO WORLD WAR 3 AND THE HISTORICAL EPOCH   Comrades, we are not living in ordinary times. We are living in a time of rupture, a time of transition, a time when the old order is decaying but refuses to die, and the new order is struggling to be born. The drive into a Third World War is not an accident. It is not a misunderstanding. It is not the result of individual leaders acting irr [ ... ]

Read more
STATEMENT OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KENYA (CPMK)
11 May 2026 07:14

  O THE WORLD ANTI IMPERIALIST PLATFORM CONFERENCE   NAIROBI, KENYA 14th MAY 2026   LL FOR INTERNATIONAL SOLIDARITY AGAINST REPRESSION, ABDUCTIONS, AND POLITICAL PERSECUTION IN KENYA   Dear comrades, revolutionary delegates, brothers and sisters in struggle,   The Communist Party Marxist Kenya extends militant greetings to all anti imperialist organisations gathered here in Nairobi. We welcome you at a critical moment in the history of Kenya, Africa, and the world anti imperialist movement. This conference is taking place at a time when imperialism is intensifying its aggres [ ... ]

Read more
The National Democratic Revolution in Kenya: Tasks of the Anti imperialist and A...
11 May 2026 07:12

  y Booker Omole General Secretary Communist Party Marxist Kenya   9th May 2026   Presented at the World Anti imperialist Front Theoretical Conference, Nairobi.   Question of Revolution in Kenya Kenya stands at a decisive historical juncture. This is not a moment of calm. This is not a moment of neutrality. This is a moment of sharpening contradictions, of deepening crisis, of rising struggle. The question before us is not whether change will come. The question is what kind of change, led by which class, in whose interests. We must speak plainly. Kenya is not an independent [ ... ]

Read more
LETTER TO THE GLOBAL NORTH
05 May 2026 14:16

 Comrades, We address you at a historical precipice. The global capitalist system, in its advanced stage of heightened imperialism, is characterized by deepening crises and escalating violence. The centers of imperial power—Washington, Brussels, London, Paris are intensifying their efforts to maintain a hegemony that is increasingly contested. In the Global South, we are the primary targets of this aggression. The mechanisms of our oppression are calculated and brutal. We are strangled by illegitimate debt, wielded not as economic aid, but as a weapon of political control by institution [ ... ]

Read more